Tel: +255752115528| Mail: info@elctmwd.org




   MWANGA BOOK SHOP         OUR PARTNERS   


  KENYA LTD  

  From : KENYA  

  Website Link : www.kenyaw.dd  

Mara baada ya Dayosisi ya Mwanga kuzaliwa au kuanzishwa Askofu mwanzilishi, Mchungaji Chedieli Elinaza Sendoro aliwekwa wakfu na kuanza majukumu yake ya kazi siku hiyi hiyo ya Tarehe 6 Novemba 2016.

Historia ya Kanisa la Kiinjili katika ukanda huu wa Pare au Vwasu ilianza mwishoni mwa karne ya19, baada ya wamisionari wa Kijerumani kutoka chama chama cha Misioni Cha Kilutheri cha Leipzig(LeipzigLutheran Missionary Society)walipofika nakuanzisha kituo kikuu cha kwanza cha Misioni Shighatini Ugweno.

Mmisionari wa kwanza au mtangulizi, Mchungaji Hans Fuchs ambae wapare walimuita (Bwana Fukudha )akitokea kituo cha misioni cha Mamba Uchagani, alifika Shighatini akasimika hema la kwanza katika ardhi ya Pare mnamo tarehe 11 mwezi julai mwaka 1900.

Pamoja na kufundisha Neno la Mungu , alianzisha shule na kufundisha watoto kusoma ,kuandika pamoja na Hesabu; alianzisha huduma ya utabibu katika zahanati , alitengeneza barabara ,alifundisha masuala ya kilimo cha kisasa pamoja na biashara , Usafi na Maendeleo ya jamii kwa ujumla.

Kutokana na juhudi zake Mmisionari Hans Fuchs na wenzake , na kwa jinsi wenyeji walivyo wapokea kwa ukarimu wamisionari hawa, Neno la Mungu pamoja na maendeleo vilichanua na kuenea Pare /Vwasu yote.



  LUTHERAN BELIVERS  

  From : TANZANIA  

  Website Link : www.jesusking.com  

Jesus is king Jesus is king Jesus is king Jesus is king Jesus is king Jesus is king Jesus is king


MFUKO WA KUDUMU WA MAENDELEO YA DAYOSISI LIPA NAMBA :  3 2 3 2 1 1   ELCT-MWANGA DIOCESE [ VODACOM ]